Lugha Nyingine
Ufaransa yatoa stempu kusherehekea Mwaka Mpya wa Jadi wa China
(Tovuti ya Gazeti la Umma) Januari 24, 2022
PARIS, Jan. 22 (Xinhua) -- Kampuni ya huduma ya posta ya Ufaransa La Poste Jumamosi ya wiki iliyopita ilitoa stempu mbili kusherehekea ujio wa Mwaka Mpya wa Jadi wa China wa chui milia utakaoanza Februari mosi.
Ikiwa na picha ya chui milia aliyejilaza kwenye mandharinyuma nyekundu, Stempu moja inatumika kwa huduma ya posta nchini Ufaransa kwa thamani ya euro 1.16.
Stempu nyingine ikiwa na picha ya chui milia anayekodolea macho mbali kwenye mandharinyuma ya bluu, ina thamani ya euro 1.65 kwa huduma ya posta ya kimataifa.
Chen Jianghong, msanii kutoka China, mbunifu wa stempu hizo, alisema chui milia hao wawili wanawakilisha nguvu na matumaini.
(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)
Kuhusu Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma