人民网首页

Simulizi

Feng Xingya (kulia), mjumbe wa Bunge la Umma la 14 la China, akifahamishwa kuhusu uondoaji na ufungaji betri kwenye kituo cha huduma ya nishati kwa magari yanayotumia umeme mjini Guangzhou, Mkoa wa Guangdong, kusini mwa China, Februari 24, 2025. (Xinhua/Liu Dawei)

Mjumbe wa Bunge la Umma la China atoa wito wa kusukuma maendeleo kwa uvumbuzi katika tasnia ya magari

Feng Xingya, mwenyekiti wa kundi la kampuni za kuunda magari la China, GAC, amekuwa akifanya kazi katika tasnia ya magari kwa miaka zaidi ya 30. Ameshuhudia maendeleo ya tasnia ya magari ya China.

Mjumbe Kamati ya 14 ya Kitaifa ya Baraza la Mashauriano ya Kisiasa la China akikagua toleo la Breli la ripoti ya kazi ya serikali kwenye kikao cha kundi la wajumbe wa sekta ya ustawi wa jamii na huduma za jamii wa Mkutano wa tatu wa Kamati ya 14 ya Kitaifa ya Baraza la Mashauriano ya Kisiasa la China, Machi 5. (Xinhua)

Ripoti ya kazi ya serikali ya China yatolewa katika Breli kusaidia wajumbe wenye ulemavu wa macho

Katika mikutano mikuu miwili ya China inayoendelea mjini Beijing, yaani mkutano wa mwaka wa Bunge la 14 la Umma la China na ule wa Kamati ya 14 ya Kitaifa ya Baraza la Mashauriano ya Kisiasa la China, toleo la Breli (maandishi ya watu wenye ulemavu wa macho) la ripoti ya kazi ya serikali ya nchi hiyo imetolewa kwa mara ya kwanza kwa wajumbe wa Baraza la Mashauriano ya Kisiasa la China. Wakati wa mchana wa jana Alhamisi, tarehe 5, Machi, mjumbe wa baraza hilo, Li Qingzhong kwenye kikao cha kikundi cha wajumbe wa sekta ya ustawi wa jamii na huduma za jamii, mahsusi aliomba kila mjumbe kuzingatia ripoti hiyo maalumu ya kazi ya serikali aliyokuwa ameishika mkononi wakati akizungumza.

Gexi Wangmu (Kulia) akifahamishwa kuhusu huduma za afya za eneo husika alipomtembelea mwanakijiji mzee katika Kijiji cha Songgang cha Mji wa Maerkang, Eneo linalojiendesha la Makabila ya Watibet na Waqiang la Aba, Mkoa wa Sichuan, kusini-magharibi mwa China, Februari 18, 2025. (Xinhua/Wang Xi)

Mjumbe wa Bunge la Umma la China adumisha mawasiliano na wakazi wazee kupitia huduma za matunzo

ABA - Gexi Wangmu, ni mjumbe wa Bunge la 14 la Umma la China, anayefanya kazi kama mkurugenzi wa kituo cha matunzo ya wazee katika Mji wa Maerkang wa Mkoa wa Sichuan, Kusini Magharibi mwa China. Akiwa ni mjumbe wa bunge hilo wa "kuzaliwa baada ya miaka ya 90", Gexi alianza maisha yake ya utumishi kama mfanyakazi wa mstari wa mbele wa huduma za matunzo ya wazee, na amejitolea kwa miaka 16 katika kazi yake hiyo.

Sun Jingnan (wa pili kushoto) akizungumza na wafanyakazi wenzake katika karakana ya CRRC Tawi la Nanjing Puzhen, Mkoa wa Jiangsu wa China, mashariki, Februari 20, 2025. (Xinhua/Li Bo)

Mjumbe wa Bunge la China na mchomeleaji vyuma mstadi anayejitoa kwa mafunzo ya mafundi vijana

NANJING - Sun Jingnan amekuwa akifanya kazi kama mchomeleaji vyuma katika Kampuni ya Vifaa vya Reli ya CRRC ya China Tawi la Nanjing kwa zaidi ya miongo mitatu, na pia shahidi wa maendeleo ya haraka ya sekta ya usafiri wa reli ya China. Akiwa amekua kutoka fundi kijana hadi kuwa mtaalamu, Sun ni mshauri na mlezi kitaaluma kwa vijana wengi wenye vipaji katika sekta hiyo ya reli.

1