BEIJING - Vijiji vya Olimpiki kwa ajili ya Michezo ya Olimpiki ya Majira ya baridi ya Beijing 2022 cha eneo la Yanqing, mjini Beijing na Zhangjiakou, Mkoa wa Hebei vilifungua milango yao kwa wanamichezo na maafisa wa timu kwa ajili ya Michezo hiyo siku ya Alhamisi ya wiki hii. Zhang Guannan, mfanyakazi wa timu ya uendeshaji wa Kijiji cha Olimpiki cha Beijing, amesema kijiji hicho kitawapokea wanamichezo 1,000 na maafisa wa timu kutoka nchi na kanda 44.
Kwa kuwa Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing imekaribia, majaribio ya mwisho ya zana na vifaa na mazoezi ya mwisho ya mchakato mzima wa michezo hiyo yanafanyika kwenye uwanja wa utoaji wa medali wa Beijing, uwanja huo uko karibu na Uwanja wa Michezo wa Taifa “Kiota cha Ndege”.
Mazoezi ya sherehe za ufunguzi wa Michezo ya Olimpiki ya Majira ya baridi ya Beijing 2022 yamefanyika kwenye Uwanja wa Taifa uitwao "Kiota cha Ndege," Januari 22, 2022. Takriban washiriki 4,000 walihusika katika mazoezi ya kila tukio la sherehe ya ufunguzi, wakijiandaa kwa sherehe ya ufunguzi itakayofanyika Februari 4.
Kijiji cha Michezo ya Olimpiki cha Zhangjiakou ( Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing na Michezo ya Olimpiki ya Walemavu ya Majira ya Baridi ya Beijing itafanyika hapa Beijing na huko Zhangjiakou, ndiyo maana kuna vijiji viwili vya michezo hiyo ) kilifunguliwa Januari 23 na kukaribisha kundi la kwanza la wakazi. Zaidi ya watu 40 wa ujumbe wa watangulizi wa michezo hiyo kutoka Australia, Uingereza, Kanada na nchi na kanda nyingine walifika na kukaa huko.