人民网首页

Mahojiano

Balozi wa Burundi nchini China Télesphore Irambona akitoa hotuba kwenye mkutano na waandishi wa habari Juni 12, 2026. (Picha/Song Ge)

Wiki ya Utamaduni wa Burundi kufanyika Beijing

Balozi wa Burundi nchini China, ambaye pia ni mwakilishi wa nchi inayoshikilia uenyekiti wa zamu wa Umoja wa Afrika, Télesphore Irambona, ametangaza kwamba Ubalozi wa Burundi mjini Beijing utafanya Wiki ya Utamaduni wa Burundi ambayo ni ya kwanza kabisa kufanyika, ikihusisha shughuli mbalimbali. Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye ofisi za Ubalozi wa Burundi Juni 12, Balozi Irambona alieleza kuwa mfululizo wa shughuli za Wiki hiyo ya Utamaduni wa Burundi zenye kaulimbiu isemayo "Ngoma Takatifu ya Burundi (Ingoma) Inapoimarisha Uhusiano wa Kiutamaduni kati ya China na Afrika" zitafanyika jijini Beijing kuanzia tarehe 28 Juni hadi tarehe 1 Julai, zikihusisha kwa sehemu kubwa maonyesho ya kiutamaduni, kongamano la uwekezaji, na maadhimisho ya miaka 64 ya Uhuru wa Burundi.

Shahidi wa Urafiki: Safari ya masomo ya Mwanafunzi Mtanzania nchini China

Chuma Mohamed Muhibu, mwanafunzi Mtanzania mwenye umri wa miaka 35, kwa sasa anasoma shahada ya uzamivu (PhD) katika Sera na Vitendo vya Elimu ya Walimu (Teacher Education Policy and Practice) katika Chuo Kikuu cha Ualimu cha Beijing nchini China. Imepita miaka saba tangu alipofika China kwa mara ya kwanza mwaka 2019 kwa ajili ya masomo yake.

Sudan na China zinafurahia uhusiano wa kimkakati wenye mizizi ya kina: Afisa wa Sudan

Mjumbe wa Baraza la Mamlaka ya Mpito la Sudan, Abdullah Yahya amesema, Sudan na China zinafurahia uhusiano uliokita mizizi ya kina uliojengwa katika uhusiano wa kimkakati na wa kunufaishana. Akizungumza katika tukio la “Asante, China” lililofanyika Port Sudan, mashariki mwa Sudan juzi Jumatatu, Yahya ameeleza mchango muhimu wa China katika miradi ya miundombinu nchini Sudan, hususan katika maendeleo ya barabara, madaraja, mabwawa na vituo vya kuzalisha umeme.

Kuielewa China | Ni hamasa gani mipango ya miaka mitano inatoa kwa Nchi za Dunia ya Kusini?

Kipindi cha "Kuielewa China", kilichoandaliwa na People's Daily Online, kinalenga kufafanua mipango, fursa, na utawala wa China, kuondoa uelewa potofu, na kuongeza uelewa wa kina na utambuzi kati ya watazamaji waChina na wa kimataifa kupitia mazungumzo ya kina kati ya wasomi wa China na wa kigeni. Uundaji wa kisayansi na utekelezaji usiositishwa wa mipango ya miaka mitano ya China vinawakilisha mbinu muhimu katika utawala wa Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) na hutumika kama dirisha muhimu kwa jumuiya ya kimataifa kuelewa ujenzi wa mambo ya kisasa wa China.

1