Mjumbe wa Baraza la Mamlaka ya Mpito la Sudan, Abdullah Yahya amesema, Sudan na China zinafurahia uhusiano uliokita mizizi ya kina uliojengwa katika uhusiano wa kimkakati na wa kunufaishana. Akizungumza katika tukio la “Asante, China” lililofanyika Port Sudan, mashariki mwa Sudan juzi Jumatatu, Yahya ameeleza mchango muhimu wa China katika miradi ya miundombinu nchini Sudan, hususan katika maendeleo ya barabara, madaraja, mabwawa na vituo vya kuzalisha umeme.
Kipindi cha "Kuielewa China", kilichoandaliwa na People's Daily Online, kinalenga kufafanua mipango, fursa, na utawala wa China, kuondoa uelewa potofu, na kuongeza uelewa wa kina na utambuzi kati ya watazamaji waChina na wa kimataifa kupitia mazungumzo ya kina kati ya wasomi wa China na wa kigeni. Uundaji wa kisayansi na utekelezaji usiositishwa wa mipango ya miaka mitano ya China vinawakilisha mbinu muhimu katika utawala wa Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) na hutumika kama dirisha muhimu kwa jumuiya ya kimataifa kuelewa ujenzi wa mambo ya kisasa wa China.