Lugha Nyingine
Tanzania: Mazingira ya uwekezaji na biashara ni salama
Serikali imesema mwamko wa biashara na uwekezaji ni mkubwa kwa sasa baada ya baadhi ya makampuni na taasisi zilizokuwa zimefunga shughuli zao kuanza kurejea, na kwamba serikali kwa sasa inapitia upya sera yake ya uwekezaji ili kuweka mazingira bora zaidi ya biashara na uwekezaji.
Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula, aliyasema hayo mwishoni mwa wiki jana jijini Dar es Salaam, alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Uholanzi nchini Tanzania,Jeroen Verheul, na kuongeza kuwa tamko la rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuhusu kuimarisha mazingira ya uwekezaji na biashara yanakuwa Rafiki.
Balozi wa Uholanzi nchini Tanzania amekiri kuwa Tanzania ina fursa na rasilimali nyingi zinazohamasisha na kuvutia biashara na uwekezaji licha ya uwepo wa maeneo machache yanayohitaji maboresho . Kulingana na balozi, endapo maeneo haya yataboreshwa, makampuni mengi kutoka ulaya yatakuja kuwekeza.
Aina nane maarufu zaidi za maua ya Yunnan hakika kuna moja inayokushangaza zaidi
Korongo wacheza kwenye uwangja wa juu hali ya viumbe yaendelea vizuri mkoani Tibet
Rasilimali ya utamaduni yasukuma mbele ujenzi wa kijiji cha kupendeza cha Luquan mjini Shijiazhuang
Mji wa Zhengzhou warudia katika hali ya kawaida ya uzalishaji na maisha
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma