Tanzania: Rais Samia afichua mpango wa kuboresha biashara ndogo

(CRI Online) Juni 17, 2021

Serikali inakusudia kufanya makutano na viongozi wa vikundi vya wajasiriamali ili kupata mpango wa kufanya biashara unaolenga kukuza makusanyo ya ushuru.

Rais Samia alitoa kauli hiyo kwa mkutano na vijana uliofanyika katika viwanja vya Nyamagana jijini Mwanza huku akithibitisha kujitolea kwa serikali kushughulikia changamoto zinazolikabili kundi hilo ikiwa ni pamoja na ukosefu wa ajira.

Mkuu wa Nchi amesema lengo la kubadilisha biashara ndogo ndogo ni kuziboresha ili kuonyesha hali ya uchumi wa kati.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha