Lugha Nyingine
China yarusha chombo kilichobeba wanaanga kwenda kituo chake kwenye anga ya juu
China jana Alhamis imerusha chombo cha Shenzhou -12 kilichobeba wanaanga watatu, ambacho kinatarajiwa kuwapeleka kwenye kituo chake cha anga ya juu cha Tiangong kwa kazi ya miezi mitatu.
Kwa mujibu wa Shirika la Anga ya Juu la China, chombo hicho kilichobebwa na roketi ya Long March-2F, kilirushwa kwenye kituo cha kurushia cha Jiuquan, kilichopo kwenye jangwa la Gobi kaskazini magharibi mwa China. Hii ni mara ya saba ya chombo cha safari kwenye anga ya juu cha China kupeleka wanaanga kwenye anga ya juu, na ni safari ya kwanza baada ya kipindi cha ujenzi wa kituo kwenye anga ya juu cha China. Pia ni safari ya kwanza baada ya miaka mitano iliyopita tangu safari ya mwisho ya chombo cha safari kwenye anga ya juu cha China.
Aina nane maarufu zaidi za maua ya Yunnan hakika kuna moja inayokushangaza zaidi
Korongo wacheza kwenye uwangja wa juu hali ya viumbe yaendelea vizuri mkoani Tibet
Rasilimali ya utamaduni yasukuma mbele ujenzi wa kijiji cha kupendeza cha Luquan mjini Shijiazhuang
Mji wa Zhengzhou warudia katika hali ya kawaida ya uzalishaji na maisha
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma