Lugha Nyingine
Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania lazindua mkakati wa Utalii
Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), limeandaa mpango mkakati wa miaka mitano unaolenga kutekelezwa kwenye maeneo saba ikiwamo kubuni na kukuza wigo wa bidhaa na mazao ya utalii ili kuongeza idadi ya watalii nchini humo.
Kamishna Uhifadhi Msaidizi Mwandamizi wa Mawasiliano wa TANAPA, Paschal Shelutete, alibainisha hayo jana kwenye semina iliyoandaliwa na shirika hilo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Dodoma.
Alisema shirika linatekeleza shughuli za uhifadhi na utalii kulingana na Mpango Mkakati wa miaka mitano (2018/19 – 2022/23) ambao umefanyiwa marejeo na kuandaa mkakati mwingine wa miaka mitano kuanzia mwaka 2021/22-2025/26.
Shelutete alisema mkakati huo unalenga kutekeleza maagizo ya serikali katika sekta ya utalii nchini. Alitaja eneo lingine litakalopewa kipaumbele kwenye mkakati huo ni kuimarisha miundombinu ya utalii hususani barabara, viwanja vya ndege, malango, magati, malazi, mawasiliano, maji na umeme.
Aina nane maarufu zaidi za maua ya Yunnan hakika kuna moja inayokushangaza zaidi
Korongo wacheza kwenye uwangja wa juu hali ya viumbe yaendelea vizuri mkoani Tibet
Rasilimali ya utamaduni yasukuma mbele ujenzi wa kijiji cha kupendeza cha Luquan mjini Shijiazhuang
Mji wa Zhengzhou warudia katika hali ya kawaida ya uzalishaji na maisha
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma