Lugha Nyingine
AfCFTA yaboresha mfumo wa malipo ili kuwezesha biashara barani Afrika
Katibu Mkuu wa Eneo la Biashara Huria la Afrika (AfCFTA), Wamkele Mene amesema, uongozi wa Eneo hilo unaboresha mfumo wa malipo ili kuwezesha biashara kati ya nchi za Afrika.
Akizungumza na Shirika la Habari la China Xinhua, Bw. Mene amesema Mfumo wa Malipo na Mapatano wa Eneo hilo (PAPSS) utaanza kutumika mwishoni mwa mwaka huu ili kuwezesha biashara kati ya nchi husika barani Afrika.
Ameongeza kuwa, mfumo huo ambao unaendelezwa mahususi kwa ajili ya malipo ya biashara kwa nchi za Afrika, unafanyiwa majaribio katika baadhi ya nchi za Afrika Magharibi.
Wakati huohuo, Mene amesema baadhi ya changamoto katika makubaliano ya biashara zimechelewesha utekelezaji kamili wa Eneo hilo barani Afrika, lakini ameeleza matumaini yake nchi nyingine zitakamilisha makubaliano yao ili kuungana na nchi kama Kenya, Afrika Kusini na Misri ambazo tayari zimeanza kufanya biashara kupitia Eneo hilo.
Aina nane maarufu zaidi za maua ya Yunnan hakika kuna moja inayokushangaza zaidi
Korongo wacheza kwenye uwangja wa juu hali ya viumbe yaendelea vizuri mkoani Tibet
Rasilimali ya utamaduni yasukuma mbele ujenzi wa kijiji cha kupendeza cha Luquan mjini Shijiazhuang
Mji wa Zhengzhou warudia katika hali ya kawaida ya uzalishaji na maisha
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma