Rais wa China asisitiza maendeleo ya sifa ya juu ya kazi ya Chama cha CPC kuhusu mambo ya kikabila

(CRI Online) Agosti 31, 2021

Rais Xi Jinping wa China amesisitiza kuimarisha hisia za jamii nzima kwa Taifa la China na kushughulikia mambo ya kikabila kwa kushikilia njia sahihi ya Ujamaa wenye umaalum wa China.

Rais Xi Jinping wa China pia alitembelea Jumba la Makumbusho la Chengde tarehe 24 Agosti, ambapo alitazama maonesho ya picha za Kumbukumu za Umoja wa Kitaifa wa Enzi ya Qing.

Rais Xi ameeleza kuwa, China ni nchi yenye makabila mbalimbali, ambayo imeundwa kuwa Taifa la China katika historia ndefu.

Mbele ya picha inayoonesha kurudi China kwa kabila la Waturhu wakati wa Enzi ya Qing, rais Xi amesema, kabila la Waturhu lilidhamiria kurudi China baada ya kutenganishwa nje kwa miaka 100, hali ambayo imeonesha ushawishi mkubwa wa Taifa la China.

Katika Wilaya inayojiendesha ya Bayinguoleng ya mkoa wa Mongolia iliyoko kwenye Mkoa unaojiendesha wa Xinjiang Uygor, wanaishi watu wengi wa vizazi vya watu wa kabila wa Waturhu. Kila mwaka tarehe 23 Juni, shughuli mbalimbali zinafanyika kwa ajili ya kukumbuka za kurudi China kwa kabila hilo. Filamu na maonesho mbalimbali pia zimeonesha moyo wao wa uzalendo na mshikamano, pamoja na imani na dhamira yao ya kithabiti.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha