Upande wa Jeshi la Guinea watangaza kuunga mkono "Kamati ya Umoja na Maendeleo ya Kitaifa"

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Septemba 09, 2021

Tarehe 7, maofisa wa ngazi mbalimbali wa jeshi la Guinea walifanya mazungumzo na kiongozi wa waasi Mamadi Dubai, na walitangaza kuunga mkono wanajeshi waasi na “Kamati ya Umoja na Maendeleo ya Kitaifa” iliyoanzishwa nao.

Kamanda wa Jeshi la Anga la Guinea, ambaye pia ni mkurugenzi wa Ofisi ya Wizara ya Ulinzi wa Taifa alisema kwenye mazungumzo kwamba, kuunga mkono wanajeshi waasi ni kwa kufikiria kulinda maslahi ya taifa na kuzuia uvamizi kutoka nje, alitumai jeshi litaendelea kulinda amani ya nchi na usalama wa jamii.

(Wahariri wa tovuti:Li Yidan,Zhao Jian)

Picha