Shehena ya pili ya chanjo za corona zinazochangiwa na China yawasilishwa Brunei

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Septemba 14, 2021

Usiku wa tarehe 12 wa huko, shehena ya pili ya chanjo za corona ambazo zinachangiwa na China imewasilishwa nchini Brunei.

Bibi Yu Hong, balozi wa China nchini Brunei na Erywan, waziri mkuu wa mambo ya nje ya Brunei walifanya hafla ya kukabidhi chanjo hizo.

Bw. Erywan akiwa kwa niaba ya serikali ya Brunei na watu wake, alishukuru serikali ya China na watu wake kutoa msaada mkubwa tena wakati Brunei ilipoathiriwa vibaya kabisa na Corona na ilipohitaji msaada kwa dharura. Alisema, katika nusu ya kwanza ya mwaka huu, shehena ya kwanza ya chanjo za corona zilichazochangiwa na China ilifanya kazi muhimu kwa kuimarisha kazi ya Brunei ya kuzuia maambukizi ya virusi vya corona.   

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha