Marekani aliye mhusika kwenye msukosuko wa Ukraine: Kuna sintofahamu nyingi kuhusu Maabara ya baiolojia ya Ukraine, lakini Marekani inataka kupuuzia mbali mambo haya

(Tovuti ya Gazeti la Umma) April 02, 2022

Tarehe 7 Machi, Wizara ya Ulinzi ya Russia ilitoa hadharani nyaraka zilizokamatwa nayo nchini Ukraine: Marekani inadhibiti maabara za baiolojia zaidi ya 30 nchini Ukraine, na maabara hizo zimepokea amri ya kuteketeza vitendanishi vyote vya kibaiolojia kuanzia Februari 24.

Upande wa Marekani ulilaumu kuwa Russia ilieneza habari zisizo za kweli. Msemaji wa Ikulu ya Marekani Jen Psaki alisema kuwa Marekani haikuhuisha na haimiliki silaha za kibaiolojia katika sehemu yoyote. Lakini Naibu Waziri wa Mambo ya Nje ya Marekani Victoria Nuland alikiri kwenye Mkutano wa kusikiliza ushahidi kuwa, nchini Ukraine kuna majengo ya utafiti wa kibaiolojia na upande wa Marekani umeshirikiana na upande wa Ukraine ili kuepusha “nyaraka za utafiti” kukamatwa na Jeshi la Russia.

Msemaji wa Ikulu ya Marekani na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje ya Marekani, ni nani anatunga uongo? Kwa kukabiliwa na ushahidi unaofichuliwa mmoja baada ya mwingine, upande wa Marekani ulijaribu kupuuzia mbali hali ya mambo kwa kusema tu hizi ni habari zisizo za kweli, kitendo chake kweli hakiwezi kuaminiwa na watu. Kama upande wa Marekani ukitaka kujithibitisha kuwa hauna uhusiano na mambo hayo, unatakiwa kuwa na msimamo wa kuwajibika na kutoa ufafanuzi wa pande zote juu ya shughuli zake za kijeshi katika utafiti wa kibaiolojia ili kuondoa sintofahamu za jumuiya ya kimataifa.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha