“Mtengenezaji wa sumu” --sababu za msiba

(Tovuti ya Gazeti la Umma) April 15, 2022

(Mchoraji wa katuni: Ma Hongliang)

Hivi karibuni, maabara ya baiolojia ya Marekani nchini Ukraine yalifuatiliwa na watu wa pande mbalimbali. Kihalisi, shughuli za kijeshi za kibaiolojia za Marekani nchini Ukraine ni moja tu ya shughuli zake zote. Wizara ya Ulinzi wa Taifa ya Marekani imedhibiti maabara 336 katika nchi 30 duniani kote kwa kisingizio cha “ushirikiano wa kupunguza hatari ya kibaiolojia” na “kuimarisha usafi wa kiumma wa dunia nzima”, na maabara hizo zimetapakaa katika sehemu za Afrika, Ulaya wa Mashariki, Asia ya Kusini Mashariki na Mashariki ya Kati. Na ajali zilitokea mara kwa mara katika maabara hizo, ambapo kuna dalili nyingi za hali ya hatari.

Tukihesabu ajali zilizotokea katika maabara za Marekani tutatambua, Marekani ni “mtengenezaji wa sumu” ambaye ni sababu za msiba, ni chanzo cha uhasama na vita. Katika karne iliyopita, Marekani iliwahi kutumia watu wenye asili ya Afrika kwa kufanya “Majaribio ya Kaswende ya Tuskegee”, ili kufanya utafiti wa kisiri juu ya madhara ya ugonjwa wa Kaswende kwa mwili wa mtu, na ilificha hali halisi ya majaribio hayo kwa miaka 40 hadi yafichuliwe na vyombo vya habari mwaka 1972; mwaka 2013, Kituo cha Lugar kilichoko Georgia cha Wizara ya Ulinzi wa Taifa wa Marekani kilianzisha majaribio ya chanjo ya kimeta, na mwaka huo maambukizi ya ugonjwa wa kimeta yalilipuka nchini Georgia; kutoka mwaka 2009 mpaka mwaka 2014, maaraba ya silaha ya kibaiolojia ya Jeshi la Marekani nchini Korea Kusini ilifanya majaribio hatari ya virusi vya kimeta kwa mara zaidi ya 15, na mwaka 2015, hata Kituo cha Kemia ya Kibaiolojia cha Marekani kilipopeleka sampuli ya virusi vya kimeta kwa kituo cha Jeshi la Marekani nchini Korea Kusini kilisababisha tukio la kusafirisha kwa makosa na kuvifanya virusi vya tauni vingie nchini Korea Kusini; hasa kituo cha kibaiolojia cha Fort Detrick nchini Marekani kinachoitwa na vyombo vya habari vya Marekani kuwa “ kituo cha kufanya majaribio haramu cha serikali ya Marekani”, ambapo ajali nyingi za kuleta hali ya hatari zilitokea kwenye kituo hicho , hivyo kilifungwa mwezi Julai, 2019......

Marekani iliyofanya vitendo vingi vibaya kama hivyo ilipofuatiliwa na kuulizwa na jumuiya ya kimataifa, ilitoa maelezo ya uwongo tu kwa kuepusha kijeuri lawama za watu kila mara. Marekani ilifanya nini katika maabara zake za kibaiolojia zilizoko sehemu mbalimbali duniani? Upande wa Marekani ungetoa ufafanuzi wazi kwa kuwajibika na kutoa jibu kwa dunia nzima.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha