Rais Xi Jinping ajibu barua kutoka wanafunzi wa Uingereza kuhusu mabadiliko ya tabianchi

(CRI Online) April 22, 2022

Picha iliyopigwa kutoka angani Agosti 19, 2020 ikionesha mitambo ya kuzalisha umeme kwa upepo kwenye eneo la Jiucaiping, Mkoa wa Guizhou wa Kusini Magharibi mwa China. (Picha/Xinhua)

Rais Xi Jinping wa China amejibu barua kutoka wanafunzi wa shule ya msingi ya Francis Holland nchini Uingereza kuhusu suala la mabadiliko ya tabianchi.

Kwenye barua yake, rais Xi amebainisha kuwa Dunia ni familia kubwa, na binadamu wote wanatoka jumuiya moja, akisema wakati mabadiliko ya tabianchi yakileta changamoto kwa binadamu wote, ushirikiano unahitajika ili kutatua suala hilo.

Rais Xi amesisitiza kuwa China inaheshimu na kupenda mazingira ya asili tangu enzi na dahari. Amesema China inatoa wito kwa jamii nzima kulinda na kuhifadhi mazingira kama watu wanavyotunza macho yao, na kujituma katika kusukuma mbele maendeleo ya kijani ili kuijenga China iwe nchi inayopendeza.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha