Rais Xi Jinping wa China ampongeza Lula da Silva kwa kuapishwa kuwa Rais wa Brazil

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Januari 03, 2023

BEIJING - Rais wa China Xi Jinping Jumatatu alituma salamu za pongezi kwa Luiz Inacio Lula da Silva kwa kuapishwa kuwa rais mpya wa Jamhuri ya Shirikisho la Brazil.

Katika pongezi lake, Rais Xi ameeleza kuwa China na Brazil ni nchi kubwa zinazoendelea zenye ushawishi wa kimataifa na masoko muhimu yanayoibukia.

Rais Xi ameongeza kwamba, nchi hizo mbili ni washirika wa pande zote wa kimkakati wanaoshiriki maslahi mapana ya pamoja na kubeba majukumu ya pamoja ya maendeleo.

Tangu kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia miaka 48 iliyopita, uhusiano kati ya nchi hizo mbili umeshuhudia maendeleo endelevu na ya kina kutokana na juhudi za pamoja za pande zote mbili, na yamekua ya kukomaa na yenye nguvu, Rais Xi amesema na kuongeza kuwa uhusiano kati ya China na Brazil umekuwa mfano wa kuigwa wa uhusiano kati ya nchi kuu zinazoendelea zenye maana tajiri na matarajio mapana.

Rais Xi pia amesema anatilia maanani sana maendeleo ya ushirikiano wa kimkakati kati ya China na Brazil, na yuko tayari kushirikiana na Lula ili kuendelea kusaidiana kithabiti katika kufuata njia ya maendeleo inayoendana na hali halisi ya nchi hizo, kuheshimu maslahi ya msingi ya kila mmoja wao, kukuza ushirikiano wao wa kivitendo, kuimarisha uratibu wa uhusiano wa pande nyingi, na kuongoza na kusukuma ushirikiano huo kwenye kiwango cha juu kwa kuangalia mtazamo wa kimkakati na wa muda mrefu, ili kufaidisha zaidi nchi hizo mbili na watu wao.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha