Njia mpya ya usafiri wa pamoja wa reli na barabara kuu yafunguliwa kupitia ukanda wa biashara wa nchi kavu na baharini

(Tovuti ya Gazeti la Umma) April 04, 2023

https://english.news.cn/20230403/b7b6ae8610d04f3bbfdc3faa8f2b879b/20230403b7b6ae8610d04f3bbfdc3faa8f2b879b_5e16b8ce-bcb4-4e98-b0b3-3a1a3636ef4f.jpg

Picha hii iliyopigwa Tarehe 3 Aprili 2023 ikionyesha treni ya mizigo ikiondoka kutoka Eneo la Jiangjin la Mji wa Chongqing, Kusini-Magharibi mwa China, ikiashiria ufunguzi wa njia mpya ya usafirishaji kupitia Ukanda Mpya wa Biashara ya Kimataifa kwenye Nchi kavu na Baharini. (Xinhua/Tang Yi)

CHONGQING - Treni ya mizigo imeondoka kutoka Eneo la Jiangjin la Mji wa Chongqing, Kusini-Magharibi mwa China siku ya Jumatatu, ikiwa ni kuashiria ufunguzi wa njia mpya ya usafirishaji kupitia Ukanda Mpya wa Biashara ya Kimataifa kwenye Nchi kavu na Baharini.

Jumla ya makontena 32 yanayobeba bidhaa kama vile salfa ya ammoniamu, sehemu za pikipiki na matairi ya pikipiki yatasafirishwa hadi Stesheni ya Kaskazini ya Baoshan katika Mkoa wa Yunnan. Bidhaa hizi zitasafirishwa kupitia barabara kuu, kutoka China kupitia bandari kwenye nchi kavu katika mji wa Ruili, kabla ya kuwasili Myanmar.

Kuanzia Januari hadi Februari mwaka huu, treni za mizigo na magari ya kubeba bidhaa kwenye Ukanda Mpya wa Magharibi kwenye Nchi kavu na Baharini kuanzia Chongqing zilisafirisha jumla ya makontena 21,000, ikiwa ni ongezeko la asilimia 46 kuliko mwaka jana. Thamani ya jumla ya bidhaa zilizosafirishwa ilifikia zaidi ya yuan bilioni 3.65 (kama dola za Kimarekani milioni 530.48), ikiwa ni ongezeko la hadi asilimia 43 kuliko mwaka uliopita.

Ukanda Mpya wa Biashara ya Kimataifa kwenye Nchi kavu na Baharini ulianzishwa mwaka 2017, ni njia ya biashara na usafrishaji iliyojengwa kwa pamoja na serikali za ngazi ya mikoa ya Magharibi mwa China na nchi wanachama wa ASEAN.

Ukanda Mpya wa Biashara ya Kimataifa kwenye Nchi kavu na Baharini umeendelea kwa kasi kwa miaka mingi, na kupanua idadi ya vituo hadi bandari 393 katika nchi na maeneo 119 kufikia mwisho wa Februari Mwaka 2023.

https://english.news.cn/20230403/b7b6ae8610d04f3bbfdc3faa8f2b879b/20230403b7b6ae8610d04f3bbfdc3faa8f2b879b_5b2c82ab-86ec-4078-a1a3-c1fe4b0720b6.jpg

Picha hii iliyopigwa Tarehe 3 Aprili 2023 ikionyesha treni ya mizigo ikiondoka kutoka Wilaya ya Jiangjin katika Manispaa ya Chongqing, Kusini-Magharibi mwa China, ikiashiria ufunguzi wa njia mpya ya usafirishaji kupitia Ukanda Mpya wa Biashara ya Kimataifa kwenye Nchi kavu na Baharini. (Xinhua/Tang Yi)

https://english.news.cn/20230403/b7b6ae8610d04f3bbfdc3faa8f2b879b/20230403b7b6ae8610d04f3bbfdc3faa8f2b879b_f84d2268-3168-4e8c-8556-5c6188cd7970.jpg

Picha hii iliyopigwa Tarehe 3 Aprili 2023 ikionyesha treni ya mizigo ikiondoka kutoka Wilaya ya Jiangjin katika Manispaa ya Chongqing, Kusini-Magharibi mwa China, ikiashiria ufunguzi wa njia mpya ya usafirishaji kupitia Ukanda Mpya wa Biashara ya Kimataifa kwenye Nchi kavu na Baharini. (Xinhua/Tang Yi)

https://english.news.cn/20230403/b7b6ae8610d04f3bbfdc3faa8f2b879b/20230403b7b6ae8610d04f3bbfdc3faa8f2b879b_153f9aae-07a6-43cc-bb60-f2067db25acc.jpg

Picha hii iliyopigwa Tarehe 3 Aprili 2023 ikionyesha treni ya mizigo ikiondoka kutoka Wilaya ya Jiangjin katika Manispaa ya Chongqing, Kusini-Magharibi mwa China, ikiashiria ufunguzi wa njia mpya ya usafirishaji kupitia Ukanda Mpya wa Biashara ya Kimataifa kwenye Nchi kavu na Baharini. (Xinhua/Tang Yi)

https://english.news.cn/20230403/b7b6ae8610d04f3bbfdc3faa8f2b879b/20230403b7b6ae8610d04f3bbfdc3faa8f2b879b_4fcc655d-d518-4a6a-a779-dff0d7965969.jpg

Picha hii iliyopigwa Tarehe 3 Aprili 2023 ikionyesha treni ya mizigo ikisubiri kuondoka kutoka Wilaya ya Jiangjin katika Manispaa ya Chongqing, Kusini-Magharibi mwa China, ikiashiria ufunguzi wa njia mpya ya usafirishaji kupitia Ukanda Mpya wa Biashara ya Kimataifa kwenye Nchi kavu na Baharini. (Xinhua/Tang Yi)

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha