

Lugha Nyingine
China yashuhudia kuongezeka kwa usafiri wa watu wengi wakati wa likizo ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, Mei Mosi
Mtoto akitumia vifaa vya Uhalisia Pepe (VR) kwenye Jumba la Makumbusho ya Sayansi na Teknolojia la Nanjing katika Mji wa Nanjing, Mkoa wa Jiangsu Mashariki mwa China, Mei 1, 2023. China imeshuhudia ongezeko la usafiri wa watu wengi wakati wa likizo ya siku tano ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, Mei Mosi ambayo ni likizo ya kwanza ya Siku ya Wafanyakazi ambapo watu wameweza kusafiri katika maeneo mbalimbali ya vivutio ya ndani na nje ya nchi tangu kuzuka kwa janga la virusi vya Korona Mwaka 2019 na nchi hiyo kuondoa masharti ya kudhibiti UVIKO-19 mapema mwaka huu. (Picha na Fang Dongxu/Xinhua)
Mtoto akiwa na furaha kwenye kanivali katika Eneo linalojiendesha la Kabila la Wahani la Mojiangous, Mkoa wa Yunnan, Kusini-Magharibi mwa China, Mei 1, 2023. (Xinhua/Hu Chao)
Picha hii ya angani iliyopigwa Tarehe 30 Aprili 2023 ikionyesha watalii wanaotembelea eneo lenye mandhari nzuri katika Mji wa Zunhua, Mkoa wa Hebei, Kaskazini mwa China. (Picha na Liu Mancang/Xinhua)
Watalii wakirusha tiara katika Mji wa Harbin, Mkoa wa Heilongjiang Kaskazini-Mashariki mwa China, Mei 1, 2023. (Xinhua/Zhang Tao)
Picha hii ya angani iliyopigwa Tarehe 1 Mei 2023 ikionyesha watalii wanaotembelea bustani ya burudani katika Wilaya ya Qianxi, Mkoa wa Hebei, Kaskazini mwa China. (Xinhua/Fan Shihui)
Picha hii ya angani iliyopigwa Tarehe 1 Mei 2023 ikionyesha watalii wakiburudika katika eneo lenye mandhari nzuri katika Eneo la Zigui, Mji wa Yichang katika Mkoa wa Hubei katikati mwa China. (Picha na Wang Huifu/Xinhua)
Picha hii ya angani iliyopigwa Tarehe 29 Aprili 2023 ikionyesha watalii wakiburudika kwenye eneo la kupiga kambi katika Mji wa Qianxi, Mkoa wa Guizhou, Kusini-Magharibi mwa China. (Picha na Fan Hui/Xinhua)
Picha hii ya angani iliyopigwa Tarehe 29 Aprili 2023 ikionyesha eneo la kupiga kambi katika Mji wa Qianxi, Mkoa wa Guizhou, Kusini-Magharibi mwa China. (Picha na Fan Hui/Xinhua)
Watalii wakitazama onyesho la kucheza ngoma kwenye Bustani ya Maonyesho ya Nanning huko Nanning, Mkoa unaojiendesha wa Kabila la Wazhuang wa Guangxi, Kusini mwa China, Aprili 30, 2023. (Xinhua/Zhou Hua)
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma