Lugha Nyingine
Waendeshaji wa biashara ya utalii kutoka China watafuta fursa kwenye soko la utalii la Zanzibar, Tanzania

Wafanyabiashara kutoka makampuni ya utalii na mashirika ya vyombo vya habari ya China wakiwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume huko Zanzibar nchini Tanzania Tarehe 12 Mei, 2023. Takriban watu 40 kutoka makampuni ya uendeshaji biashara za utalii na mashirika ya vyombo vya habari ya China waliwasili Zanzibar siku ya Ijumaa katika hatua ya kuanza ziara ya ufahamisho ili kufungua soko la utalii la Tanzania kwa China. “Mpango huu unalenga kufungua soko letu kwa China,” amesema Hafsa Mbamba, Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Utalii ya Zanzibar nchini Tanzania. (Picha na Nurdin Pallangyo/Xinhua)
DAR ES SALAAM - Takriban watu 40 kutoka makampuni ya uendeshaji biashara za utalii na mashirika ya vyombo vya habari ya China waliwasili Zanzibar siku ya Ijumaa katika hatua ya kuanza ziara ya ufahamisho ili kufungua soko la utalii la Tanzania kwa China.
“Mpango huu unalenga kufungua soko letu kwa China,” amesema Hafsa Mbamba, Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Utalii ya Zanzibar nchini Tanzania.
Akizungumza mara baada ya kupokea kundi hilo la wachina wanaotembelea Zanzibar kwa mara ya kwanza baada ya janga la UVIKO-19, Mbamba amesema kundi hilo kutoka mikoa mbalimbali nchini China litapata fursa ya kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii.
“Wageni hao kutoka China wataonyeshwa utamaduni wetu, urithi wetu na utalii wa fukwe na vivutio vingine mbalimbali vitakavyowawezesha kuvitangaza pindi watakaporejea China,” amesema Mbamba alipowapokea wageni hao kutoka China kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, visiwani Zanzibar, Tanzania.
Amesema wageni hao kutoka China watakuwa na mazungumzo ya biashara kwa biashara na wenzao wa Zanzibar wakati wa uwepo wao visiwani humo.

Wafanyabiashara kutoka makampuni ya utalii na mashirika ya vyombo vya habari ya China wakiwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume huko Zanzibar nchini Tanzania Tarehe 12 Mei, 2023. (Nurdin Pallangyo/Xinhua)
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma



