Mji wa Shanghai, Mashariki mwa China waboresha mazingira ya biashara kwa kutumia huduma muhimu za serikali

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Mei 17, 2023
Mji wa Shanghai, Mashariki mwa China waboresha mazingira ya biashara kwa kutumia huduma muhimu za serikali
Wananchi wakishughulikia biashara kwenye Eneo la Majaribio la Biashara Huria la Eneo Maalum la Lingang la Shanghai, Mashariki mwa China, Mei 12, 2023. (Xinhua/Ma Ning)

SHANGHAI - Shanghai ilikuwa imetoa jumla ya ripoti maalum 4,163 kuhusu muamana ya kampuni za biashara kufikia Aprili 30 mwaka huu, na kutoa nyongeza za uthibitisho zaidi ya 74,000 kwa kampuni husika za kutokuwa na rekodi ya makosa ya kukiuka sheria na taratibu. Utaratibu rahisi wa maombi ulioratibiwa kwa ufanisi umesaidia kampuni kuokoa nguvu kazi, nyenzo na wakati kwa biashara katika mji huo.

Kuanzia Machi 1, kampuni za biashara za Shanghai zinahitaji tu kuingia katika tovuti maalum na kupata nakala ya ripoti inayozalishwa kiotomatiki kuhusu uthibitisho wa imani juu ya biashara yao, ambayo itasema kuwa kampuni haina ukiukaji wa sheria na taratibu katika muda uliochaguliwa.

Kampuni zitaweza kutoa ripoti maalum kuhusu hali ya muamana zao zenyewe ili kuthibitisha kama zina ukiukaji wowote katika kategoria 41 ndani ya maeneo ya usimamizi ya Shanghai.

Kategoria 23 za kwanza zimeanza kubainishwa mwezi huu wa Machi, na zinahusisha usimamizi wa soko, mazingira ya ikolojia, usimamizi wa miji na usafiri, huku kategoria nyingine 18 zitaanza kutekelezwa kuanzia Januari 2024 na kuendelea, kwa mujibu wa Liu Yanhao, Naibu Mkurugenzi wa Ofisi ya Haki ya Manispaa ya Shanghai.

"Kutokana na kujifunza jinsi ya kutuma maombi ya kupata uthibitisho wa muamana mtandaoni na kuchagua muda na nyanja inayohitaji uthibitisho, tulipokea ripoti maalum iliyotolewa kiotomatiki chini ya nusu saa, ambayo ilikuwa ni yenye ufanisi mkubwa," amesema mkurugenzi wa idara ya majaribio ya kampuni inayojikita mahsusi katika dawa za maumbile ya mwili.

Utawala kwa mujibu wa sheria unatoa mazingira mazuri ya biashara. Shanghai inaendelea kuboresha mazingira ya biashara kupitia sera nyingi za upendeleo. Tangu Mwaka 2019, Shanghai imekuwa ikitafuta njia nyingi mbadala za kutotoza adhabu za kiutawala kwa ukiukaji mdogo, na kukamilisha mara kwa mara orodha ya ukiukaji wa sheria, ambayo inaruhusu kampuni nyingi kufanya kazi na kuwekeza Shanghai bila wasiwasi zaidi.

Matumizi halisi ya uwekezaji wa kigeni huko Shanghai katika robo ya kwanza ya Mwaka 2023 yalifikia dola za Kimarekani bilioni 7.8, ikiwa ni ongezeko la asilimia 28.1 kuliko mwaka uliopita. Naibu Mkurugenzi wa Kamati ya Biashara ya Manispaa ya Shanghai Bw. Zhang Guohua amesema, Jumla ya makao makuu 907 ya kikanda ya kampuni za kimataifa na vituo 538 vya utafiti na maendeleo vilivyowekezwa na mitaji kutoka nje vimeanzishwa mjini Shanghai.

(Wahariri wa tovuti:Shixi,Zhao Jian)

Picha