Lugha Nyingine
Watafiti wataka juhudi zaidi zitumike kuwalinda mbwa mwitu wa Ethiopia walio hatarini
Chuo Kikuu cha Kiebrania cha mjini Yerusalem kimesema, utafiti umethibitisha uwepo wa mbwa mwitu wa Ethiopia miaka milioni 1.5 iliyopita.
Katika utafiti huo uliochapishwa katika jarida la Nature Communications Biology, watafiti kutoka Chuo Kikuu hicho wakishirikiana na wenzao kutoka Hispania, Marekani, Italia na Ethiopia, walitafiti kwa pamoja mabaki ya fuvu la chini la mbwa mwitu wa Ethiopia lililogunduliwa mwaka 2017 katika eneo la Melka Wakena.
Kwa mujibu wa utafiti huo, mabaki hayo ni ya miaka milioni 1.5 iliyopita, matokeo yanayokinzana na madai ya awali kuwa mbwa mwitu wa Ethiopia walikwenda Afrika wakitokea nchi za Ulaya na Asia miaka karibu 20,000 iliyopita.
Habari Picha: Mandhari ya maeneo yanayozunguka Mto Bahe katika Mji wa Xi'an, China
Katika Picha: Watu wakivuna matunda ya bluberi katika Kijiji cha Wengbao, Mkoa wa Guizhou wa China
Habari Picha: Ndege wakionekana Lhasa, huko Tibet, Kusini Magharibi mwa China
Katika Picha: Tazama mandhari ya Mji wa Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC)
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma