UM: Idadi ya vifo vilivyosababishwa na mvua kubwa DRC yafikia watu 443

(CRI Online) Mei 24, 2023

Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA) siku ya Jumanne imesema, idadi rasmi ya vifo kutokana na mvua kubwa iliyosababisha mafuriko na maporomoko ya udongo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imeongezeka hadi kufikia watu 443, huku mamia ya watu wakijeruhiwa na wengi hawajulikani walipo.

OCHA pia imesema, mahitaji ya dharura kwa sasa ni makazi na chakula kwa manusura, na ukarabati wa barabara na madaraja pia ni muhimu ili waathirika waweze kufikiwa.

(Wahariri wa tovuti:Shixi,Zhao Jian)

Picha