Kenya yazindua kituo cha kwanza cha kuchaji mabasi ya umeme

(CRI Online) Mei 25, 2023

Kenya jana ilizindua kituo chake cha kwanza cha kuchaji mabasi ya umeme ya umma, katika juhudi za nchi hiyo kuelekea katika usafiri wa kutumia nishati safi.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya BasiGo ya Kenya Bw. Jit Bhattacharya amesema, kituo cha kuchaji kwa haraka cha DC chenye uwezo wa kuchaji mabasi sita ya umeme kwa wakati mmoja, kimetengenezwa chini ya usaidizi wa shirika la umeme linalomilikiwa na serikali, Kenya Power.

Bw. Bhattacharya amesema, kituo hicho ni cha kwanza kuunganishwa na huduma mpya ya ushuru kwa magari yanayotumia umeme iliyopitishwa mwezi Machi mwaka huu, ambayo inatoa umeme kwa bei nafuu kwa magari hayo kuchaji nyakati za usiku wakati nchi ina ziada kwenye utoaji wa nishati endelevu.

(Wahariri wa tovuti:Shixi,Zhao Jian)

Picha