China yaitaka Marekani irekebishe makosa na kuonyesha udhati kwa ajili ya mazungumzo ya kijeshi

(CRI Online) Mei 31, 2023

China imeitaka Marekani irekebishe haraka makosa yake kwa vitendo, na kuonyesha udhati kwa ajili ya mazungumzo kati ya majeshi ya nchi hizo mbili.

Hayo yamesemwa na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China Mao Ning alipozungumzia hoja iliyotolewa na Marekani kwamba China imekataa ombi la Marekani la kufanyika kwa mazungumzo kati ya mawaziri wa ulinzi wa nchi hizo mbili pembezoni mwa Mkutano wa Kilele wa Usalama wa Asia au Mazungumzo ya Shangri-La chini Singapore.

Mao Ning amesema Marekani inafahamu vya kutosha ni kwa nini mazungumzo ya kijeshi kati ya China na Marekani yanakabiliwa na changamoto, ni lazima Marekani iheshimu mamlaka, usalama na mambo yanayofuatiliwa na China na kuweka mazingira mazuri kwa ajili ya mazungumzo hayo.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha