Chuo Kikuu cha Algiers nchini Algeria chazindua "Rafu ya Vitabu vyenye maudhui ya China" ili kuhimiza mabadilishano ya kitamaduni

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Juni 05, 2023

Balozi wa China nchini Algeria Li Jian (Kulia) na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Algiers 1 Fares Mokhtari wakizindua "Rafu ya Vitabu vyenye maudhui ya China" huko Algiers, Algeria, Juni 4, 2023. (Xinhua)

Balozi wa China nchini Algeria Li Jian (Kulia) na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Algiers 1 Fares Mokhtari wakizindua "Rafu ya Vitabu vyenye maudhui ya China" huko Algiers, Algeria, Juni 4, 2023. (Xinhua)

ALGIERS - Mradi wa "Rafu ya Vitabu vyenye maudhui ya China" ambao unalenga kuimarisha mabadilishano ya kitamaduni na ushirikiano wa sekta ya elimu kati ya China na Algeria umezinduliwa katika Chuo Kikuu cha Algiers 1 siku ya Jumapili.

"Rafu ya Vitabu vyenye maudhui ya China" ina vitabu 460 vilivyoandikwa kwa Lugha za Kiarabu, Kifaransa na Kiingereza, vyenye maudhui yanayohusiana na masuala ya kisiasa, kiuchumi, kijamii na kitamaduni ya China. Vitabu vyote vimetolewa na kampuni ya mafuta ya China Sinopec.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na Balozi wa China nchini humo Li Jian, Mkuu wa Chuo Kikuu cha Algiers 1 Fares Mokhtari, Mwakilishi Mkuu wa Sinopec Tawi la Afrika Wei Dong na mwakilishi wa Wizara ya Nishati na Madini ya Algeria, Fatiha Relimi.

Balozi Li amesema ana imani kwamba vitabu vilivyotolewa vitatumika kama dirisha la kupata maarifa ya kina ya China na kuwasaidia wanafunzi kupata uelewa wa kina wa China.

Kwa upande wake, Fares Mokhtari ameielezea rafu hiyo ya vitabu kama "daraja la maarifa na utamaduni ili kuimarisha uhusiano wa pande mbili kati ya China na Algeria," huku akiongeza kuwa "chuo kikuu hicho kinatafuta ushirikiano zaidi wa kivitendo na taasisi na vyuo vikuu vya China."

Naye Wei Dong ameelezea matumaini yake kwamba vitabu hivyo "vitachangia maendeleo ya chuo kikuu na ukuaji wa wanafunzi, akisisitiza kuwa "Sinopec itaendelea kujitolea kwa wajibu wake wa kijamii huku ikiunga mkono uchumi endelevu na anuai wa Algeria."

Balozi wa China nchini Algeria Li Jian (Kulia) na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Algiers 1 Fares Mokhtari wakizindua "Rafu ya Vitabu vyenye maudhui ya China" huko Algiers, Algeria Juni 4, 2023. (Xinhua)

Balozi wa China nchini Algeria Li Jian (Kulia) na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Algiers 1 Fares Mokhtari wakizindua "Rafu ya Vitabu vyenye maudhui ya China" huko Algiers, Algeria Juni 4, 2023. (Xinhua)

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha