

Lugha Nyingine
Gavana wa Hawaii aonya kuwa waathiriwa 10 hadi 20 zaidi wa moto wa nyika wanaweza kupatikana kwa siku baada ya watu 96 kufariki
Picha hii iliyotolewa na Kaunti ya Maui Agosti 10, 2023 ikionyesha nyumba zilizoteketezwa kwa moto mkubwa kwenye Kisiwa cha Maui, Hawaii, Marekani. (Kaunti ya Maui/ Xinhua)
LOS ANGELES - Josh Green, Gavana wa Jimbo la Hawaii nchini Marekani, ameonya katika mahojiano siku ya Jumatatu kwamba waathiriwa 10 hadi 20 zaidi wa moto wa nyika wanaweza kupatikana kwa siku huku watafutaji wa waathirika wakiendelea kupenya kwenye magofu ya nyumba zilizoungua kwenye kisiwa cha Maui huko Hawaii.
Idadi ya watu waliofariki kutokana na moto huo wa nyika unaokumba sehemu za kisiwa hicho cha pili kwa ukubwa cha Hawaii imeongezeka hadi 96.
Ndiyo moto mkubwa zaidi kuwahi kutokea katika kipindi cha zaidi ya karne moja katika historia ya kisasa ya Marekani, ukipita Moto wa Kambi uliolipuka Novemba 8, 2018 huko California na kuua angalau watu 85.
Mioto mikubwa imekaribia kuharibu kabisa mji wa kihistoria wa Lahaina, sehemu maarufu ya watalii huko Maui na hapo zamani ilikuwa mji mkuu wa Ufalme wa Hawaii. Ni nyumbani kwa wakazi wapatao 13,000.
Green amekiambia kituo cha matangazo ya televisheni na redio cha Marekani, CBS katika mahojiano yaliyorekodiwa ambayo yamerushwa Jumatatu kwamba kuna uwezekano wa kuwa na majeruhi na vifo zaidi.
Wakaazi wote wa Lahaina ama wamekimbia makazi yao au kuangamia kwa moto, gavana huyo amenukuliwa akisema kwenye kituo cha CBS, lakini itachukua siku 10 kuthibitisha idadi kamili ya vifo kwani wafanyakazi wanaweza kupata "watu 10 hadi 20 kwa siku labda hadi kumaliza."
Mkuu wa Polisi wa Maui John Pelletier alisema katika mkutano na wanahabari Jumamosi kwamba mbwa wa unusaji walikuwa wametafuta asilimia 3 tu ya maeneo yaliyoathiriwa.
Moto wa Lahaina, ambao ni moto wa nyika ulioangamiza Lahaina, ulikuwa umedhibitiwa kwa asilimia 85 kufikia Jumapili usiku, Kaunti ya Maui ilisema katika taarifa yake mpya.
Picha hii iliyotolewa na Kaunti ya Maui Agosti 10, 2023 ikionyesha nyumba zilizoteketezwa kwa moto mkubwa kwenye Kisiwa cha Maui, Hawaii, Marekani. (Kaunti ya Maui/ Xinhua)
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma