

Lugha Nyingine
Huawei yaahidi kuendeleza ujumuishi wa kidijitali nchini Kenya kwa kupitia uvumbuzi wa kiteknolojia
(CRI Online) Oktoba 12, 2023
Kampuni ya mawasiliano ya China, Huawei, imeahidi kuisaidia Kenya kuongeza kasi yake ya ujumuishi wa kidijitali, na kuhakikisha kupanua upatikanaji wa majukwaa na huduma za moja kwa moja mtandaoni kwa kutoa uvumbuzi wa kiteknolojia.
Ofisa Mkuu wa Teknolojia wa Kampuni ya Huawei Kanda ya Kusini mwa Afrika, Tony Li, amesema hayo katika mkutano wa kikanda uliofanyika mjini Nairobi, Kenya. Amesema nchi hiyo tayari imeshuhudia maendeleo dhahiri katika muongo uliopita, kwa kuanza kutumia mitandao ya teknolojia za 4G na 5G.
Amesema teknolojia ni msingi unaoruhusu kila mjasiriamali kufungua biashara, kila mwalimu kufundisha wanafunzi bila kujali sehemu waliko duniani, na kila mwananchi kupata huduma bora za afya.
(Wahariri wa tovuti:Shixi,Zhao Jian)
Kuhusu Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma