Idadi ya watalii waliofika Zanzibar yazidi milioni moja

(CRI Online) Novemba 01, 2023

Kamisheni ya Utalii ya Zanzibar nchini Tanzania imesema idadi ya watalii wa kigeni waliotembelea kisiwa hicho imeongezeka kwa asilimia 110.28 kutoka 260,644 wa mwaka 2020 hadi 548,503 mwaka 2022 huku, na idadi hiyo ikijumuishwa na watalii wa ndani imefikia lengo la juu la kufikia watalii milioni moja (1,000,000) ifikapo Mwaka 2025, ambalo liliwekwa na mamlaka hiyo.

Waziri wa Utalii na Urithi wa Zanzibar Bw. Simai Mohammed Said, amethibitisha kuwa idadi ya watalii imekaribia kufikia milioni moja.

Licha ya changamoto zilizotokana na janga la Covid-19, miaka michache iliyopita imeshuhudia mabadiliko kamili kwenye sekta ya utalii.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha