Rais Xi apokea na kusikiliza ripoti kutoka kwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Hong Kong

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Desemba 19, 2023

Rais Xi Jinping akikutana na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mkoa wa Utawala Maalum wa Hong Kong wa China (HKSAR) John Lee, ambaye yuko katika ziara ya kikazi mjini Beijing, China, Desemba 18, 2023. (Xinhua/Li Xueren)

Rais Xi Jinping akikutana na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mkoa wa Utawala Maalum wa Hong Kong wa China (HKSAR) John Lee, ambaye yuko katika ziara ya kikazi mjini Beijing, China, Desemba 18, 2023. (Xinhua/Li Xueren)

BEIJING - Rais Xi Jinping wa China amekutana na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mkoa wa Utawala Maalum wa Hong Kong wa China (HKSAR) John Lee, ambaye yuko katika ziara ya kikazi mjini Beijing, ambapo Rais Xi amesikiliza ripoti kutoka kwa Lee kuhusu hali ya sasa ya Hong Kong na kazi ya serikali ya HKSAR na kupongeza kazi ya Lee katika mwaka uliopita akisema kwamba ameiongoza serikali ya HKSAR katika kubeba majukumu na kutoa matokeo mazuri.

Serikali ya HKSAR imelinda kwa uthabiti usalama wa nchi, imeufanyia mageuzi utaratibu wa mabaraza ya utawala wa maeneo ya Hong Kong, imekamilisha vizuri Uchaguzi wa Kawaida wa mabaraza ya utawala wa maeneo, na kuwezesha Hong Kong kuondokana na athari za janga la UVIKO-19 na kuelekea ufufukaji wa pande zote, Rais Xi amesema.

Rais Xi amesema, Serikali ya HKSAR imedumisha hadhi na faida maalum za mkoa huo, imeimarisha vichocheo vya maendeleo na kufanya juhudi kubwa za kuondoa matatizo na shida kubwa za watu, haya yote yameimarisha hali ya HKSAR inayoelekea kuwa nzuri,na kuhimiza Hong Kong kuingia katika kipindi kipya cha kurudisha utaratibu wake na kuendelea kustawi. Serikali Kuu ya China itatekeleza kikamilifu, kwa uthabiti na kwa usahihi sera ya "nchi moja, mifumo miwili" kwa muda mrefu na kutekeleza kikamilifu sera ya "wazalendo kusimamia Hong Kong," Rais Xi amesema.

Rais Xi Jinping akikutana na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mkoa wa Utawala Maalum wa Hong Kong wa China (HKSAR) John Lee, ambaye yuko katika ziara ya kikazi mjini Beijing, China, Desemba 18, 2023. (Xinhua/Li Xueren)

Rais Xi Jinping akikutana na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mkoa wa Utawala Maalum wa Hong Kong wa China (HKSAR) John Lee, ambaye yuko katika ziara ya kikazi mjini Beijing, China, Desemba 18, 2023. (Xinhua/Li Xueren)

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha