

Lugha Nyingine
Manufaa makubwa yavutia njia mpya ya meli ya moja kwa moja kati ya Tanzania na China
Kupitia Kampuni ya Usafirishaji wa Majini ya Korea (KMTC), Tanzania inatarajiwa kufaidika kwa kiasi kikubwa kutokana na uzinduzi wa njia mpya ya meli ya moja kwa moja kati ya China na Bandari ya Dar es Salaam.
Huduma hii mpya inatarajiwa kupunguza kwa kiasi kikubwa muda wa mizigo kuwasili kutoka China kutoka wiki sita (siku 42) hadi wiki tatu (siku 21), na kuongeza ufanisi wa biashara za Tanzania. Ujio wa KMTC katika Bandari ya Dar es Salaam umefanikishwa kutokana na kukamilika kwa Mradi wa Mlango wa Majini wa Dar es Salaam (DMGP).
Mradi huo wa uboreshaji uliogharimu Dola za Kimarekani milioni 440.4 (sawa na trilioni 1.12/-) utaruhusu meli kubwa kama KMTC kufika kwa urahisi na kutia nanga katika Bandari ya Dar es Salaam.
Akitoa maoni yake katika hafla ya uzinduzi wa njia hiyo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi ya Tanzania Prof Godius Kahyarara, amesisitiza umuhimu wa DMGP katika kuvutia shughuli za KMTC.
Amesema njia hiyo ni hatua kubwa kwa bandari hiyo na ni fursa kubwa kwa ustawi wa biashara kati ya Tanzania na nchi za Asia.
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma