Takwimu kutoka kampuni ya utalii zaonesha watalii wa China wamefanya utalii katika miji zaidi ya 1,700 Duniani

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Februari 18, 2024

Watu wakiwa kwenye Stesheni ya Kusini ya Beijing tarehe 17, Februari. (Picha na Xing Guangli/China)

Watu wakiwa kwenye Stesheni ya Kusini ya Beijing tarehe 17, Februari. (Picha na Xing Guangli/China)

Qunar.com, jukwaa la utalii la mtandao la China jana tarehe 17 lilitoa takwimu zikionesha kuwa, katika likizo ya mwaka mpya wa jadi wa China mwaka huu, nyayo za watalii wa China zimefika miji 1,754 katika nchi 115 duniani.

Nchi hizo 115 ni pamoja na Ethiopia na Madagascar barani Afrika; Uruguay katika bara la Amerika Kusini; Lituanie, Monaco, na Malte katika bara la Ulaya na nchi nyingine mbalimbali. Kwenye Qunar.com, oda za hoteli za ng’ambo wakati wa likizo zimeongezeka kwa mara 4.7 kuliko kipindi kama hicho mwaka jana, na uagizaji wa tiketi za ndege za usafiri wa kimataifa umeongezeka kwa mara 14.

Singapore, Malaysia na Thailand zilizosamehe visa hivi karibuni kwa watalii wa China zimepata ongezeko kubwa la oda za safari likizoni. Kwenye jukwaa la Qunar.com, uagizaji wa tiketi za ndege kutoka China hadi Singapore wakati wa likizo ya mwaka mpya wa jadi wa China umeongezeka kwa mara 29 kuliko likizo hiyo ya mwaka jana.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha