Lugha Nyingine
Mfalme wa Jordan aonya juu ya kupanuka kwa mgogoro ya Gaza katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani
Mfalme Abdullah II wa Jordan (Kati) akikutana na Rais wa Palestina Mahmoud Abbas (kushoto) mjini Amman, Jordan mnamo Februari 25, 2024. (Kasri la Kifalme la Hashemite/ Xinhua)
AMMAN - Mfalme Abdullah II wa Jordan ameonya siku ya Jumapili kwamba kuendelea kwa vita huko Gaza katika mwezi mtukufu wa Ramadhani kunaweza kuhatarisha kupanuka kwa mgogoro huo.
Mfalme Abdullah ameyasema hayo mjini Amman alipokutana na Rais Mahmoud Abbas wa Palestina, ambapo ametoa wito wa kufanyika juhudi kubwa zaidi ili kufikia usimamishaji vita wa mara moja na wa kudumu huko Gaza, na kulinda raia wasio na hatia, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kasri la Kifalme la Hashemite.
Mfalme huyo amebainisha kuwa Jordan itaendelea kutoa misaada ya kibinadamu, uungaji mkono, na matibabu kwa watu wa Gaza, taarifa hiyo imeongeza.
Amesisitiza Jordan inapinga majaribio yoyote ya kutenganisha Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na Ukanda wa Gaza, huku akitaka kuendelea kwa uratibu wa Nchi za Kiarabu kutafuta suluhu ya haki kwa suala la Palestina kwa kuzingatia suluhu ya nchi mbili.
Kwa upande wake Abbas, ametoa pongezi kwa misimamo thabiti ya Jordan kuhusu mgogoro kati ya Kundi la Hamas na Israel akisisitiza haja ya kuendeleza uratibu na mashauriano ya karibu kati ya pande hizo mbili ili kuwezesha harakati ya Wapalestina na kulinda maeneo matakatifu katika mji huo wa Gaza.
Sherehe ya "Kuonyesha Buddha" yafanyika katika Hekalu Kaskazini Magharibi mwa China
Watu wa kabila la Wagelao washerehekea Sikukuu ya Maolong huko Guizhou, Kusini Magharibi mwa China
Wakulima kote China wawa na pilika nyingi za uzalishaji wa kilimo wakati Siku ya Yushui yakiwadia
Ndege C919 ya China yashiriki mazoezi ya Maonyesho ya Anga ya Singapore
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma