Timu ya madaktari wa China nchini Zimbabwe yaimarisha ushirikiano wa kudumu wa afya

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Machi 13, 2024

Waziri wa Afya na Malezi ya Watoto wa Zimbabwe Dk. Douglas Mombeshora (Kati, mbele) akiwa katika picha ya pamoja na madaktari wa Kundi la 20 la Timu ya Madaktari wa China baada ya hafla ya kuwatunuku nishani mjini Harare, Zimbabwe, Machi 11, 2024. (Xinhua/Zhang Baoping)

Waziri wa Afya na Malezi ya Watoto wa Zimbabwe Dk. Douglas Mombeshora (Kati, mbele) akiwa katika picha ya pamoja na madaktari wa Kundi la 20 la Timu ya Madaktari wa China baada ya hafla ya kuwatunuku nishani mjini Harare, Zimbabwe, Machi 11, 2024. (Xinhua/Zhang Baoping)

HARARE - Wakati Zimbabwe ikiwaaga madaktari kumi na moja wa Kundi la 20 la Timu ya Madktari wa China kwa nishani na hotuba za kugusa moyo katika hafla iliyofanyika Harare siku ya Jumatatu, timu mpya ya madaktari kutoka China iko tayari kuleta hali mpya ya ushirikiano wa kudumu wa afya.

Wakiwa waliwasili mwaka mmoja uliopita katika Hospitali ya Parirenyatwa mjini Harare kutoka Mkoa wa Hunan wa China, timu hiyo inayomaliza muda wake ilitoa huduma za matibabu katika idara mbalimbali, ikiwa ni pamoja na utoaji wa tiba za jumla, tiba za wagonjwa mahututi na tiba za dawa za jadi za China.

Maafisa kutoka Ubalozi wa China nchini Zimbabwe, ujumbe wa Kamati ya Afya ya Mkoa wa Hunan, na maafisa kutoka Wizara ya Afya ya Zimbabwe walihudhuria hafla, inayopongeza huduma ya madaktari hao ambayo inabeba urafiki kati ya nchi hizo mbili.

"Kuja kutoa huduma nchini Zimbabwe kunajumuisha moyo wa kujitoa sana ambako wanaishi mbali na familia na marafiki zao kwa mwaka mzima. Tunathamini dhamira yenu isiyoyumba ya kuokoa maisha ya watu," Makamu Rais wa Zimbabwe Constantino Chiwenga amesema katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Waziri wa Afya na Huduma ya Mtoto wa Zimbabwe, Dk. Douglas Mombeshora.

Ameipongeza timu hiyo iliyomaliza muda wake kwa kutoa huduma bora za afya kwa jamii za wenyeji.

Pia ametambua kiwango na utaalamu wao mbalimbali, ambao ni muhimu kwa ajili ya kujenga uwezo na mafunzo ya wanafunzi wa udaktari.

"Mara nyingi timu za madaktari zimejaza baadhi ya mapungufu yetu na kuleta mawazo mapya kwenye mifumo yetu. Kwa kutambua utaalamu huo, tumeamua kupeleka Timu za Madaktari wa China kwa Kundi la Hospitali za Parirenyatwa, hospitali kuu ya kisasa ya afya ya nchi yetu, ambako fursa za kufanya kazi na wataalam wenyeji na kutoa mafunzo kwa wanafunzi wa udaktari," amesema.

Katika hotuba yake, Kaimu Balozi wa China nchini Zimbabwe Cheng Yan ameipongeza timu hiyo iliyomaliza muda wake kwa kukamilisha kazi yake kwa mafanikio na kukaribisha kundi hilo jipya.

"Kundi la 21 la Madaktari wa China limewasili wiki iliyopita. Ninaamini litaendeleza moyo wa Timu ya Madaktari wa China, kuendelea na kazi nzuri na kutoa mchango mkubwa katika ushirikiano wa afya kati ya China na Zimbabwe," amesema.

Katika hotuba yake ya kuaga, mkuu wa timu hiyo inayomaliza muda wake, Ouyang Bin, alikumbusha shughuli 14 za mashauriano ya kiafya na kimatibabu bila malipo zilizoandaliwa katika jamii, shule, na vituo vya watoto yatima, zikifika majimbo yote 10 ya Zimbabwe.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha