Msaada wa Chakula wa serikali ya China kwa Ukanda wa Gaza wa Palestina kuwasili Port Said nchini Misri

(CRI Online) Machi 21, 2024

Ubalozi wa China nchini Misri umesema katika taarifa yake kwa vyombo vya habari kwamba ili kupunguza changamoto ya hali ya kibinadamu katika Ukanda wa Gaza, serikali ya China inaendelea kutoa msaada kwa Palestina kadri inavyoweza.

Kwa mujibu wa ubalozi huo, China imetoa msaada wa fedha taslimu kwa awamu kadhaa na kwa sasa inawasilisha shehena mbili za chakula, vifaa tiba na mahitaji mengine muhimu ya kibinadamu kwa Ukanda wa Gaza kupitia Misri.

Ubalozi umesema, wakati wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani, China imezidisha juhudi zake za kutoa chakula kwa Ukanda wa Gaza na kwamba Machi 28, msaada wa mchele wa China kwa Palestina utawasili Port Said, nchini Misri, na kusafirishwa hadi Gaza kupitia kivuko cha Rafah.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha