Lugha Nyingine
Afrika kutumia teknolojia ya anga ya juu kusaidia maendeleo yake
Kamishna wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Uvumbuzi wa Umoja wa Afrika, Mohammed Belhocine amesema, Afrika inakaribia kuanzisha Mamlaka ya Anga ya Juu ya Afrika (AfSA) kwa lengo la kutumia teknolojia ya anga ya juu kusaidia maendeleo ya bara hilo.
Amesema sera ya Umoja wa Afrika inapendekeza kuanzishwa kwa Mamlaka hiyo, na hatua zimeshachukuliwa katika mwaka uliopita na mwaka huu kuhakikisha kuwa Mamlaka hiyo inaanzishwa.
Ameweka wazi kuwa, maandalizi ya kuanzishwa kwa Mamlaka hiyo ambayo makao yake makuu yatakuwa jijini Cairo, Misri, yamekamilika kwa asilimia 90, na kwamba mfumo wa uongozi wake umeridhiwa na nchi wanachama wa Umoja wa Afrika.
Amesisitiza kuwa, kanuni ya msingi ya sera ya anga ya juu ya Afrika ni matumizi ya amani ya rasilimali za anga ya juu.
Shughuli ya kuadhimisha Siku ya Mashua ya Qintong 2024 yafanyika Jiangsu, China
Watu watoa heshima kwa marehemu kabla ya siku ya Qingming katika Mji wa Beijing, China
Msanii wa Ethiopia abuni sanaa kutokana na ufunuo wa kitabu maarufu cha China “Yi Jing”
Treni yaendeshwa katikati ya maua karibu na sehemu ya Juyongguan ya Ukuta Mkuu wa Beijing
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma