Lugha Nyingine
Sudan Kusini yaanza maandalizi ya uchaguzi mkuu utakaofanyika Desemba
Sudan Kusini imetangaza kuwa itaanza maandalizi ya uchaguzi wa wabunge uliopangwa kufanyika mwezi Desemba mwaka huu, ukiwa ni wa kwanza tangu nchi hiyo ipate uhuru wake.
Kufuatia kumalizika kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe mwaka 2018 na kupata uhuru wake mwaka 2011, Sudan Kusini awali ilipanga kufanya uchaguzi huo kabla ya mwezi Februari mwaka jana, lakini serikali ya mpito ya nchi hiyo na upande wa upinzani walikubaliana kuahirisha hadi mwishoni mwa mwaka 2024.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Sudan Kusini Abednego Akok Kacuol amewaambia wanahabari jijini Juba kuwa, serikali imetoa fedha kwa Tume hiyo kuanza mchakato wa uchaguzi, na kwamba wameandaa mpango ambao kama utaridhiwa na wadau, uandikishaji wapiga kura utaanza mwezi Juni.
Watu wakitazama kupatwa kwa jua kikamilifu kote Amerika Kaskazini
Shughuli ya kuadhimisha Siku ya Mashua ya Qintong 2024 yafanyika Jiangsu, China
Watu watoa heshima kwa marehemu kabla ya siku ya Qingming katika Mji wa Beijing, China
Msanii wa Ethiopia abuni sanaa kutokana na ufunuo wa kitabu maarufu cha China “Yi Jing”
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma