Lugha Nyingine
Huawei yatoa mafunzo kwa roboti katika maonyesho ya wanafunzi nchini Kenya
Kampuni ya Huawei ya China imetangaza kuwa, darasa la kidijitali linaloitwa DigiTruck linalotoa mafunzo ya ujuzi wa kidijitali kwa jamii maskini barani Afrika, litatoa mafunzo ya papo kwa hapo kwa njia ya roboti katika Maonyesho ya 60 ya Sayansi na Ufundi ya Kenya yaliyoanza Jumanne wiki hii.
Kampuni hiyo imesema katika taarifa yake jana Jumanne kuwa, wanafunzi wa shule za sekondari wanatarajiwa kupata fursa ya kujifunza na kushiriki mafunzo hayo kama sehemu ya shughuli hiyo ya wiki nzima.
Katika taarifa yake hiyo iliyotolea jijini Nairobi, kampuni hiyo imesema inafurahi kuwa sehemu ya shughuli hiyo, ambayo inaendana na ahadi yake ya kuboresha fursa za mafunzo ya kidijitali kwa wanafunzi nchini Kenya.
Maonyesho ya Sayansi na Ufundi ya Kenya ni tukio la kila mwaka linalotumika kuonyesha miradi na mawazo ya ubunifu ya wanafunzi wa shule za sekondari nchini humo.
Watu wakitazama kupatwa kwa jua kikamilifu kote Amerika Kaskazini
Shughuli ya kuadhimisha Siku ya Mashua ya Qintong 2024 yafanyika Jiangsu, China
Watu watoa heshima kwa marehemu kabla ya siku ya Qingming katika Mji wa Beijing, China
Msanii wa Ethiopia abuni sanaa kutokana na ufunuo wa kitabu maarufu cha China “Yi Jing”
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma