Namna gani vyombo vya kupikia chakula vya Wachina vilionekana miaka 5,000 iliyopita?

(Tovuti ya Gazeti la Umma) April 25, 2024

Miaka 5,300 hadi 4,300 iliyopita, kulikuwa na ustaarabu wa Liangzhu kwenye eneo la Ziwa Taihu katika sehemu ya chini ya Mto Yangtze, Kusini mwa China. Ustaarabu huo ulikuwa ni wa mapema zaidi kugunduliwa nchini China.

Makumbusho ya Ustaarabu wa Liangzhu yaliyopo eneo la Yuhang la Mji wa Hangzhou, China yanasimuliza simulizi ya mafanikio ya ustaarabu na mambo ya kijamii ya kipindi cha Liangzhu. Ujuzi wa tasnia ya ufinyanzi wa vyombo vya udongo wakati huo ulikuwa tayari umeendelea sana. Hebu fuatana na kamera tutazame na kuthamini pamoja vyombo vya udongo vya kupikia chakula vilivyofinyangwa na WaLiangzhu wa kale wa miaka 5,000 iliyopita.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha