Toleo la Kiingereza la kitabu kuhusu ufafanuzi wa Xi Jinping juu ya BRI lachapishwa

(Tovuti ya Gazeti la Umma) April 29, 2024

BEIJING - Toleo la Kiingereza la kitabu cha ufafanuzi wa Xi Jinping juu ya Pendekezo la Ukanda Mmoja, Njia Moja (toleo la Mwaka 2023) kimechapishwa na Shirika la Kitaifa la Uhariri na Uchapishaji la China.

Kitabu hicho kitatolewa nchini na nje ya China, imesema taarifa rasmi iliyotolewa siku ya Jumapili.

Kitabu hicho ni mkusanyiko wa maelezo 78 muhimu kuhusu Pendekezo la Ukanda Mmoja, Njia Moja (BRI) aliyotoa Xi Jinping, Katibu Mkuu wa Kamati Kuu ya Chama cha CPC kuanzia Septemba 2013 hadi Novemba 2023.

Kitabu hiki kimehaririwa na Taasisi ya Utafiti wa Historia ya Chama na Maandishi muhimu ya Kamati Kuu ya CPC na toleo hilo la Kiingereza pia limetafsiriwa na taasisi hiyo.

Kitabu hicho kinatarajiwa kusaidia wasomaji wa kigeni kuelewa vyema dhana, hatua, malengo na mafanikio ya BRI na kutoa mchango mkubwa katika kuhimiza ushirikiano wa kimataifa chini ya BRI, imesema taarifa hiyo.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Renato Lu)

Picha