Rais Xi Jinping kufanya ziara nchini Ufaransa, Serbia na Hungary kuanzia Mei 5 hadi 10

(Tovuti ya Gazeti la Umma) April 29, 2024

BEIJING –Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China, Hua Chunying leo Jumatatu ametangaza kuwa, kutokana na mwaliko wa Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa, Rais Aleksandar Vučić wa Serbia, na Rais Tamás Sulyok na Waziri Mkuu Viktor Orbán wa Hungary, Rais Xi Jinping wa China atafanya ziara nchini Ufaransa, Serbia na Hungary kuanzia Mei 5 hadi 10.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Renato Lu)

Picha