Katika Mwongo mmoja wa Uendeshaji, Treni ya China-Ulaya (Wuhan) Yasafirisha Mizigo ya Yuan Bilioni 98.2

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Juni 04, 2024

Katika miaka ya hivi karibuni, magari mengi zaidi na zaidi yanayotumia nishati mpya yaliyozalishwa mkoani Hubei, China yamesafirishwa kuuzwa nchi za nje kupitia treni ya China-Ulaya (Wuhan). Bei ya usafirishaji huo ni sehemu ya moja ya tano ya usafirishaji wa anga, na mtandao wa huduma yake unafika karibu bara zima la Asia-Ulaya, Eurasia.

Treni hiyo ya China-Ulaya imekuwa ikifanya kazi kwa miaka 10 tangu izinduliwe. Hadi kufikia mwisho wa mwezi Mei, thamani ya bidhaa zilizosafirishwa nayo imefikia Yuan bilioni 98.2 (sawa na Dola bilioni 13.55 hivi za Marekani).

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha