

Lugha Nyingine
Wataalamu wa kigeni kusaidia kuchunguza ajali ya ndege ya Malawi
(CRI Online) Juni 18, 2024
Rais Lazarus Chakwera wa Malawi ametangaza siku ya Jumapili kwamba serikali ya Malawi itaalika wataalamu wa kigeni kusaidia kuchunguza chanzo cha ajali ya ndege iliyosababisha kifo cha makamu rais wa nchi hiyo Bw. Saulos Chilima na maofisa wengine.
Akiongea kwenye mazishi ya kitaifa, Rais Chakwera amesema wataalam wenyeji wanaendelea na uchunguzi, na kusisitiza umuhimu wa uchunguzi wa kina ili kutoa majibu yanayaowasumbua watu wa Malawi na yeye mwenyewe.
Serikali imetoa wito wa kuomboleza kwa amani huku kukiwa na baadhi ya dalili za mvutano kufuatia nadharia za njama zinazoenea juu ya ajali hiyo.
(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)
Kuhusu Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma