Kipyegon na Kipchoge wagonga vichwa vya habari kwa kuwemo kwenye timu ya riadha ya Olimpiki ya Kenya

(CRI Online) Juni 18, 2024

Mabingwa mara mbili wa Olimpiki Faith Kipyegon na Eliud Kipchoge wameifanya timu ya riadha ya Kenya kwenye Michezo ya Olimpiki ya Paris 2024 kugonga vichwa vya habari kufuatia kukamilika kwa Majaribio ya Olimpiki ya siku mbili.

Hadi kufikia sasa, Kamati ya Michezo ya Olimpiki ya Kenya imethibitisha wanariadha 37 watakaokwenda Paris, wanaume 22 na wanawake 15, huku kila upande ukiwa na wanariadha wa akiba. Hata hivyo, hicho si kikosi cha mwisho, kwa kuwa wanariadha wengine waliokidhi vigezo vya mchujo wa kumaliza katika nafasi mbili bora kwenye Majaribio wataruhusiwa kufikia kiwango cha mchujo wa Olimpiki kabla ya tarehe ya mwisho Julai 15 ya kugonga tiketi zao.

Akiwa ana tatizo la jeraha la msuli wa paja, Kipyegon, bingwa wa olimpiki ya Rio 2016 na Tokyo 2020 wa mbio za mita 1,500 kwa wanawake, atashiriki mara mbili nchini Ufaransa, baada ya kufuzu katika mashindano yake ya mbio za mita 5,000 katika mbio za kwanza za msimu wake.

Kando na wawili hao, kijana Emmanuel Wanyonyi ni miongoni mwa watarajiwa wengine wa kusisimua wa Kenya mjini Paris. Siku ya Jumamosi, alijitahidi na kufika namba 3 kwenye orodha ya wanariadha wanaume ya muda wote ya wakimbiaji wa mita 800.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha