Maofisa kutoka nchi mbalimbali za Afrika wasifu matokeo ya Mkutano wa hivi karibuni wa CPC

(CRI Online) Julai 26, 2024

Maofisa kutoka nchi mbalimbali za Afrika wanaohudhuria Jukwaa la 7 la Watu wa China na Afrika wamesifu matokeo ya mkutano wa 3 wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) uliomalizika hivi karibuni.

Katika mkutano wa jukwaa hilo unaofanyika Changsha, mkoa wa Hunan, katikati ya China, maofisa hao wamesema, ni muhimu sana kwa China na Afrika kutafuta kwa pamoja njia ya maendeleo kuelekea ujenzi wa mambo ya kisasa, na kuongeza kuwa vyama vya siasa na mashirika ya kiraia katika nchi za Afrika yako tayari kuimarisha ushirikiano na China ili kusaidia kujenga jumuiya ya China na Afrika yenye mustakabali wa pamoja.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha