

Lugha Nyingine
Mgogoro wa Sudan waacha watoto zaidi milioni 15 nje ya mfumo wa shule
(CRI Online) Novemba 13, 2024
Katibu Mkuu wa Baraza la Taifa la Ustawi wa Watoto la Sudan Bw. Abdul Qadir Abdullah Abu amesema watoto zaidi milioni 15 nchini Sudan wako nje ya mfumo wa shule.
Akiongea mjini Port Sudan Bw. Abu amevishutumu Vikosi vya Mwitikio wa Haraka (RSF) kwa ukiukaji wa kimfumo dhidi ya haki za watoto, akidai kuwa wanamgambo hao wameteka nyara watoto zaidi 2,500.
Ameongeza kuwa watoto karibu 3,000 wameuawa wakiwa ukimbizini, na watoto zaidi ya 8,000 wamekuwa wakitumikishwa na vikosi hivyo kwenye mapigano.
Bw. Abu amesema watoto ndiyo "kundi lililo hatarini zaidi" na wanahitaji mifumo ya ulinzi.
(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)
Kuhusu Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma