

Lugha Nyingine
Abiria wanusurika kwenye ajali ya treni kugongana na lori Kusini mwa Zambia
(CRI Online) Desemba 25, 2024
Abiria wa treni moja wamenusurika bila kujeruhiwa baada ya treni yao kugongana na lori kwenye eneo la Choma kusini mwa Zambia jana Jumanne.
Ajali hiyo imetokea katika makutano ya barabara na reli, baada ya treni iliyokuwa ikielekea Kaskazini kugongana na lori na trela lililobeba vigae vya sakafu likielekea Afrika Kusini.
Ofisa mahusiano wa Shirika la Reli Zambia, Sombe Longwani-Ngo’nga, amesema uchunguzi wa awali umedokeza kuwa dereva wa lori alishindwa kusimama mbele ya makutano na kusababisha ajali hiyo.
(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)
Kuhusu Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma