

Lugha Nyingine
Mlipuko wa Ebola watokea tena nchini Uganda
Wizara ya Afya ya Uganda imetangaza jana kwamba ugonjwa wa Ebola umeibuka tena nchini humo baada ya miaka miwili, ambapo muuguzi mmoja katika Hospitali ya Rufaa ya Mulago iliyoko Kampala, amefariki kutokana na ugonjwa huo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya nchini humo, Bibi Diana Atwine amesema, matokeo ya vipimo kutoka maabara yalionyesha kuwa muuguzi huyo aliambukizwa virusi vya Ebola vya Sudan na hadi sasa, watu 45 waliowasiliana naye kwa karibu, ikiwemo familia yake na wafanyakazi wa matibabu, wametengwa kwa uangalizi.
Shirika la Afya Duniani (WHO) limetoa taarifa jana likisema, limetenga dola za Marekani milioni moja kutoka kwa fedha husika za dharura kwa ajili ya kukabiliana na mlipuko huo, na linapanga kupeleka vifaa vya matibabu nchini Uganda.
Shughuli mbalimbali za kusherehekea Mwaka Mpya wa Jadi wa China zafanyika katika Nchi Nyingi
Muonekano wa Kisiwa cha Weizhou katika Mkoa wa Guangxi, Kusini mwa China
Hafla ya Kukaribisha Panda wa China yafanyika katika Bustani ya Wanyama ya Adelaide, Australia
Shughuli mbalimbali zafanyika sehemu mbalimbali China kukaribisha Mwaka Mpya ujao wa Jadi wa China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma