

Lugha Nyingine
China kuweka ushuru wa ziada kwa baadhi ya bidhaa za Canada baada ya uchunguzi dhidi ya kubagua bidhaa
BEIJING - China imetangaza leo Jumamosi kwamba itaweka ushuru wa ziada kwa baadhi ya bidhaa zinazoagizwa kutoka Canada kwenye msingi wa uamuzi wa uchunguzi dhidi ya kubagua bidhaa.
Serikali ya China imesema, mara moja kuanzia Machi 20, ushuru wa ziada wa asilimia 100 utatozwa kwa mafuta ya rapa, keki za mafuta na mbaazi zinazotoka Canada, huku bidhaa za baharini na nyama ya nguruwe zikitozwa ushuru wa ziada wa asilimia 25.
Uamuzi huo umekuja baada ya uchunguzi wa China dhidi ya kubagua bidhaa, ambao umebaini kuwa hatua zuizi za Canada dhidi ya baadhi ya bidhaa za China zimevuruga utaratibu wa kawaida wa biashara na kuathiri haki na maslahi halali ya kampuni za China.
Watu mjini Lhasa, China wafanya maandalizi ya sikukuu ijayo ya Mwaka Mpya wa Watibet
Mandhari na wanyama katika Hifadhi ya Taifa ya Nairobi, Kenya
Habari Picha: Kituo cha Matengenezo yote ya Ndege katika sehemu moja mjini Haikou, China
Dunhuang katika Mkoa wa Gansu wa China yakaribisha maendeleo mapya
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma