Tanzania yazindua kanuni ya uongezaji virutubisho kwenye chakula

(CRI Online) April 27, 2025

Serikali ya Tanzania imezindua rasmi kanuni ya uongezaji virutubisho kwenye chakula ya mwaka 2024, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kihistoria ulioanzishwa ili kuharakisha mapambano dhidi ya utapiamlo na kufanya marekebisho ya viwango vya usalama wa chakula nchini Tanzania.

Hafla ya uzinduzi huo imefanyika mkoani Ruvuma, ikiongozwa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Bw. Exaud Kigahe, pamoja na viongozi wakuu wa kitaifa na kikanda, wawakilishi kutoka mashirika ya kimataifa, wadau wa afya na lishe, wasindikaji wa chakula, wadau kutoka sekta mbali mbali na wawakilishi wa kijamii.

Sheria hii mpya inagusa wasindikaji wote wakubwa na wadogo wa bidhaa za unga wa mahindi, unga wa ngano, mafuta ya kula na chumvi, wote wanatakiwa kuongeza virutubisho (vitamin na madini) kwenye bidhaa hizo.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha