

Lugha Nyingine
Serengeti, Zanzibar, Kilimanjaro miongoni mwa vivutio vya utalii vya Tanzania washindi katika Tuzo za Utalii Duniani
Tanzania imeibuka kinara wa utalii wa Afrika kwenye Tuzo za Utalii Duniani (World Travel Awards 2025), zilizofanyika Jumamosi mjini Dar es Salaam.
Wizara ya Maliasili na Utalii ya Tanzania imesema Tanzania si tu imekuwa mwenyeji wa hafla ya mwaka huu ya utoaji tuzo hizo, lakini pia imeweka historia na kufanikiwa kuvunja rekodi kwa kupata tuzo 27 kuhusu mandhari yake ya kuvutia, sekta ya huduma za utalii, na taasisi za kipekee za utalii.
Miongoni mwa tuzo hizo ni pamoja na zile za eneo linalovutia zaidi kwa utalii, bodi ya utalii inayoongoza, na mbuga ya wanyama inayoongoza.
Taarifa iliyotolewa na wizara ya maliasili na utalii ya Tanzania inaonesha kuwa vivutio vya kitalii vilivyotambuliwa katika tuzo hizo ni Mlima Kilimanjaro, Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, fukwe safi za Zanzibar na Hifadhi ya Taifa ya Kitulo.
Kituo cha mafunzo cha Bajiquan mkoani Hebei, China chakaribisha wanafunzi kutoka Russia
Picha: Mandhari ya mbuga katika majira ya joto mkoani Gansu, China
Bustani ya Kimataifa ya Pump Track ya Shenyang, China: Utambulisho Mpya wa Michezo Mjini
Ukumbi wa Kuutazama Mji wa “Kilele cha Tianjin” wa China wafunguliwa rasmi kwa umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma